Sunday, September 2, 2012

MSHINDI BSS 2009 PASCAL CASSIAN KUZINDUA ALBAMU YAKE YA INJILI UWANJA WA FISI LEO.

Na.Mwandishi Wetu
Mshindi wa shindano la Bongo Star Search (BSS) 2009 Pascal Cassian atazindua albamu yake ya nyimbo za injili iitwayo Yasamehe Bure leo katika Uwanja wa Fisi.
Albamu hiyo itakayokuwa na nyimbo kama vile Chuki ya Nini, Nikumbuke na Mimi, Jina la Yesu, Mafuriko, Pesa, Baba na Usilie.
Akizungumzia albamu hiyo alisema kuwa ina lenga kuwarudisha waliopotea kwa Mungu kwa kuwapatia ujumbe wa neno la Mungu kwa njia ya nyimbo.
Alisema kuwa akiwa kama kijana ameamua kutumia muda, nguvu na akili zake nyingi katika kumwimbia na kumsifia Mungu na hivyo ameamua kuwafikishia vijana, watoto na watu wazima ujumbe kupitia nyimbo.
Pia akizungumzia sababu ya kuzindulia albam yake katika eneo la uwanja wa Fisi alisema kuwa kutokana na sifa mbaya ya eneo hilo ameamua ambapo limekuwa likifahamika kama uwanja wa dhambi kutokana matukio mbalimbali ambayo yanafanyika mahala hapo.
Alisema kuwa mgeni rasmi anatarajia kuwa Jaji Mkuu wa shindano la Epiq Bongo Star Search (EBSS) Ritha Paulsen ambae ndie alieibua kipaji chake kupitia shindano hilo mwaka 2009 wakati likiitwa BSS.
Uzinduzi huo pia utasindikizwa na waimbaji wengine ambao ni Martha Mwaipaja, Sifa John, Joseph Kaka, Beatrice na wengineo wengi.
Albamu hiyo ambayo ameirekodia katika studio mbalimbali imemchukua miezi mienne kuiandaa na itauzwa kwa shilingi 10000/=.
“ Mimi kwanza ninamshukuru Mungu kwa kuniongoza mpaka kufikia hatua hii ya kuzindua albamu yangu na ameweza kunifikisha hapa kupitia programu ya BSS ambapo ndipo nilionekana uwezo wangu wa kuimba na kushinda na kumbe ilikuwa ndio mwanzo wa safari yangu ya kumtumikia Mungu” alisema Cassian.

No comments:

Post a Comment